MISS TZ AKIRI KUTEMBEA NA KONDOM KWENYE MKOBA SAA 24!


Na Jelard Lucas
MISS Tanzania 2011, Salha Israel ameweka bayana bila ya woga wowote kuwa, kwenye pochi yake hakaukiwi na mipira ya kiume ‘kondom’, Amani linakupa kila kitu kinagaubaga.

Salha alisema hayo, juzi Jumanne katika mahojiano maalum, chumba cha habari cha Magazeti Pendwa Bongo, Global Publishers, Bamaga – Mwenge jijini Dar es Salaam.

HABARI KAMILI
Katika mahojiano hayo, Salha aliwekwa mtu kati ambapo alifafanua ishu hiyo pamoja na mambo mengine ndani na nje ya urembo, bila kusahau tasnia ya sinema ambayo kwa sasa ameingia kwa miguu miwili.

Swali la msingi lililozaa jibu hilo ni pale alipoulizwa kama aliwahi kutoa mimba tangu alipoanza kuelea kwenye bahari ya mapenzi, ambapo alikana kisha akafafanua: “Mimba! Weeeee.... hapana. Sijawahi kupata wala kutoa mimba.”

Akaongeza: “Mimi natumia kondom bwana, mimba itaingia wapi hapa!”
AMANI: Kama ukienda kwa jamaa na akawa hana kondom unafanyaje?
SALHA: Na kwa nini asiwe nayo? Lakini siyo tatizo sana, ndiyo maana mimi huwa nakuwa nazo kwenye pochi muda wote. Nikijua nakwenda kwa jamaa, basi zinakuwa tayari.

Sitaki kisingizio, kama atakuwa nazo fine (sawa) but (lakini) akiwa hana natoa zangu. Unajua mimi ndiye nitakayeingia kwenye matatizo ndiyo maana nakuwa makini mwenyewe.

AMANI: Kwa hiyo hata sasa hivi hapo unazo kondom kwenye pochi yako?
SALHA: (Anacheka) Hapana, hapana... kwa sasa sina na hii ni kwa sababu sina mtu muda huu ila nikiwa naye huwa siachi kuzibeba muda wote.

1 comment:

  1. Slots Guru - Casino - JeMHub
    Casino - Free 통영 출장안마 Casino Bonus - 춘천 출장안마 No deposit bonus for casinos in India. 양주 출장마사지 You can be 제주 출장안마 sure that slot machines are coming to India as well, 나주 출장안마 even for Indian players

    ReplyDelete